Zaburi 41:1-4 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Heri mtu anayewajali maskini;Mwenyezi-Mungu atamwokoa wakati wa shida.

2. Mwenyezi-Mungu atamlinda na kumweka hai,naye atafanikiwa katika nchi;Mungu hatamwacha makuchani mwa maadui zake.

3. Mwenyezi-Mungu atamsaidia awapo mgonjwa,atamponya maradhi yake yote.

4. Nami nilisema: “Unifadhili, ee Mwenyezi-Mungu,unihurumie maana nimekukosea wewe.”

Zaburi 41