Zaburi 3:4-8 Biblia Habari Njema (BHN)

4. Nakulilia kwa sauti, ee Mungu,nawe wanisikiliza kutoka mlima wako mtakatifu.

5. Nalala na kupata usingizi,naamka tena maana wewe ee Mwenyezi-Mungu wanitegemeza.

6. Sitayaogopa maelfu ya watu,wanaonizingira kila upande.

7. Uje ee Mwenyezi-Mungu!Niokoe ee Mungu wangu!Wewe wawavunja mataya maadui zangu wote;wawavunja meno waovu wasinidhuru.

8. Mwenyezi-Mungu ndiwe uokoaye;uwape baraka watu wako.

Zaburi 3