Zaburi 2:8-12 Biblia Habari Njema (BHN)

8. Niombe nami nitakupa mataifa yawe urithi wako,na dunia nzima kuwa mali yako.

9. Utawaponda kwa fimbo ya chuma;utawavunja kama chungu cha mfinyanzi!’”

10. Sasa enyi wafalme, tumieni busara;sikilizeni onyo hili, enyi watawala wa dunia.

11. Mtumikieni Mwenyezi-Mungu kwa uchaji;

12. msujudieni na kutetemeka;asije akakasirika, mkaangamia ghafla;kwani hasira yake huwaka haraka.Heri yao wote wanaokimbilia usalama kwake!

Zaburi 2