Zaburi 18:47-50 Biblia Habari Njema (BHN)

47. Yeye ameniwezesha kulipiza kisasi;na kuyashinda mataifa chini yangu.

48. Ameniokoa kutoka kwa maadui zangu,akanikuza juu ya wapinzani wangu,na kunisalimisha mbali na watu wakatili.

49. Kwa hiyo nitakutukuza kati ya mataifa,ee Mwenyezi-Mungu nitaliimbia sifa jina lako.

50. Mungu humjalia mfalme wake ushindi mkubwa;humwonesha fadhili zake huyo mteule wake,naam, humfadhili Daudi na wazawa wake milele.

Zaburi 18