Zaburi 18:3-13 Biblia Habari Njema (BHN)

3. Namwita Mwenyezi-Mungu astahiliye sifa anisaidie,nami naokolewa kutoka kwa maadui zangu.

4. Kamba za kifo zilinizingira,mawimbi ya maangamizi yalinivamia;

5. kamba za kuzimu zilinizinga,mitego ya kifo ilinikabili.

6. Katika taabu yangu nilimwita Mwenyezi-Mungu,nilimlilia Mungu wangu anisaidie.Aliisikia sauti yangu hekaluni mwake;kilio changu kilimfikia masikioni mwake.

7. Hapo dunia ikatetemeka na kutikisika;misingi ya milima ikayumbayumba,kwani Mungu alikuwa amekasirika.

8. Moshi ulifuka kutoka puani mwake,moto uunguzao ukatoka kinywani mwake;makaa ya moto yalilipuka kutoka kwake.

9. Aliinamisha anga, akashuka chini;na wingu jeusi chini ya miguu yake.

10. Alipanda kiumbe chenye mabawa akaruka;akapaa kasi juu ya mabawa ya upepo.

11. Alijifunika giza pande zote,mawingu mazito yaliyojaa maji yalimzunguka.

12. Umeme ulimulika mbele yake;kukatokea mawinguni mvua ya mawe na makaa ya moto.

13. Mwenyezi-Mungu alinguruma kutoka mbinguni;Mungu Mkuu akatoa sauti yake,kukatokea mvua ya mawe na makaa ya moto.

Zaburi 18