24. Mahali pa kupuria patajaa nafaka,mashinikizo yatafurika divai na mafuta.
25. Nitawarudishia miaka ile iliyoliwa na nzige,kila kitu kilicholiwa na tunutu, parare na matumatu,hilo jeshi kubwa nililowaletea!
26. Mtapata chakula kingi na kutosheka;mtalisifu jina la Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu,aliyewatendea mambo ya ajabu.Watu wangu, kamwe hawatadharauliwa tena.
27. Mtatambua kwamba mimi nimo miongoni mwenu,enyi Waisraeli;kwamba mimi Mwenyezi-Mungu,ndimi Mungu wenu wala hakuna mwingine.Watu wangu, kamwe hawatadharauliwa tena.
28. “Kisha hapo baadayenitaimimina roho yangu juu ya binadamu wote.Watoto wenu wa kike na wa kiume watatabiri,wazee wenu wataota ndoto,na vijana wenu wataona maono.