Yeremia 50:1-5 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Neno la Mwenyezi-Mungu alilosema kwa njia ya nabii Yeremia kuhusu nchi ya Babuloni na nchi ya Wakaldayo:

2. “Tangazeni kati ya mataifa,twekeni bendera na kutangaza,Msifiche lolote. Semeni:‘Babuloni umetekwa,Beli ameaibishwa.Merodaki amefadhaishwa;sanamu zake zimeaibishwa,vinyago vyake vimefadhaishwa.’

3. “Kwa maana, taifa kutoka kaskazini limefika kuushambulia; litaifanya nchi yake kuwa uharibifu. Hakuna atakeyeishi humo; watu na wanyama watakimbia mbali.

4. “Siku hizo na wakati huo, nasema mimi Mwenyezi-Mungu, watu wa Israeli na watu wa Yuda watakusanyika pamoja na kurudi wakilia huku wananitafuta mimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wao.

5. Watauliza njia ya kwenda Siyoni, huku nyuso zao zimeelekea huko, wakisema, ‘Njoni!’ Nao watajiunga na Mwenyezi-Mungu katika agano la milele ambalo kamwe halitasahauliwa.

Yeremia 50