Yeremia 48:27-30 Biblia Habari Njema (BHN)

27. Kumbuka Moabu ulivyomcheka Israeli. Je, alikamatwa pamoja na wezi, hata ukawa unatikisa kichwa chako kila ulipoongea juu yake?

28. “Enyi wenyeji wa Moabu,tokeni mijini, mkakae mapangoni!Mwigeni njiwa ajengaye kiota penye genge.

29. Tumesikia juu ya kiburi cha Moabu;Moabu ana majivuno sana.Tumesikia juu ya kujiona, kiburi na majivuno yake;tumesikia jinsi anavyojigamba moyoni.

30. “Nami Mwenyezi-Mungu nasema:Najua ufidhuli wake;Majivuno yake ni ya bure,na matendo yake si kitu.

Yeremia 48