Yeremia 48:17-20 Biblia Habari Njema (BHN)

17. Mwomboleezeni Moabu, enyi jirani zake wote,na nyote mnaomjua vizurisemeni: ‘Jinsi gani fimbo ya nguvu ilivyovunjwa,naam fimbo ile ya fahari!’

18. Enyi wenyeji wa Diboni:Shukeni kutoka mahali penu pa fahari,mkaketi katika ardhi isiyo na maji.Maana mwangamizi wa Moabu,amefika kuwashambulia;amekwisha haribu ngome zenu.

19. Enyi wakazi wa Aroeri,simameni kando ya njia mtazame!Mwulizeni anayekimbia na anayetoroka:‘Kumetokea nini?’

20. Moabu imeaibishwa maana imevunjwa;ombolezeni na kulia.Tangazeni kando ya mto Arnoni,kwamba Moabu imeharibiwa kabisa.

Yeremia 48