1. Mwenyezi-Mungu asema: “Wakati utakuja ambapo nitakuwa Mungu wa jamaa zote za Israeli nao watakuwa watu wangu.
2. Mimi Mwenyezi-Mungu nasema:Watu walionusurika kuuawaniliwaneemesha jangwani.Wakati Israeli alipotafuta kupumzika,
3. mimi Mwenyezi-Mungu nilimtokea kwa mbali.Nami nimekupenda kwa mapendo ya daima,kwa hiyo nimeendelea kuwa mwaminifu kwako.
4. Nitakujenga upya nawe utajengeka,ewe Israeli uliye mzuri!Utazichukua tena ngoma zakoucheze kwa furaha na shangwe.