1. Neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Mwenyezi-Mungu:
2. “Mimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wa Israeli, nasema hivi: Yaandike katika kitabu maneno yote niliyokuambia.
3. Maana siku zaja ambapo nitawarudishia fanaka zao watu wangu wa Israeli na Yuda na kuwarudisha katika nchi niliyowapa wazee wao, nao wataimiliki. Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”
4. Haya ndiyo mambo aliyosema Mwenyezi-Mungu kuhusu watu wa Israeli na Yuda:
5. “Mimi Mwenyezi-Mungu nasema hivi:Kumesikika kilio cha hofusauti ya kutisha wala si ya amani.