Yeremia 23:22-27 Biblia Habari Njema (BHN)

22. Kama wangalihudhuria baraza langu,wangaliwatangazia watu wangu maneno yangu,wakawageuza kutoka katika njia zao mbovu,na kutoka katika matendo yao maovu.

23. “Mimi ni Mungu aliye karibu, si Mungu aliye mbali.

24. Je, mtu aweza kujificha mahali pa siri hata nisiweze kumwona? Hamjui kuwa mimi Mwenyezi-Mungu nipo kila mahali, mbinguni na duniani? Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.

25. Mimi nimeyasikia maneno waliyosema hao manabii wanaotabiri uongo kwa jina langu, wakisema, ‘Nimeota ndoto, nimeota ndoto!’

26. Itakuwa hivyo mpaka lini? Hao manabii wataendelea mpaka lini kupotoka moyo; kutabiri uongo na udanganyifu wa mioyo yao wenyewe?

27. Kwa ndoto zao hizo wanapanga kuwafanya watu wangu wanisahau mimi kama baba zao walivyonisahau, wakamwendea Baali!

Yeremia 23