20. Mbele ya watu hawa,nitakufanya ukuta imara wa shaba.Watapigana nawe,lakini hawataweza kukushinda,maana, mimi niko pamoja nawe,kukuokoa na kukukomboa.Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.
21. Nitakuokoa mikononi mwa watu waovu,na kukukomboa makuchani mwa wakatili.”