8. Tunaye dada mdogo,ambaye bado hajaota matiti.Je, tumfanyie nini dada yetusiku atakapoposwa?
9. Kama angalikuwa ukuta,tungalimjengea mnara wa fedha;na kama angalikuwa mlango,tungalimhifadhi kwa mbao za mierezi.
10. Mimi nalikuwa ukuta,na matiti yangu kama minara yake.Machoni pake nalikuwakama mwenye kuleta amani.
11. Solomoni alikuwa ana shamba la mizabibu,mahali paitwapo Baal-hamoni.Alilikodisha kwa walinzi;kila mmoja wao alilipa vipande elfu vya fedha.