Walawi 4:7-13 Biblia Habari Njema (BHN)

7. Kuhani atachukua sehemu ya damu na kuzipaka pembe za madhabahu ya kufukizia ubani wa harufu nzuri, mbele ya Mwenyezi-Mungu katika hema la mkutano. Damu inayobaki ataimwaga chini kwenye tako la madhabahu ya kuteketezea sadaka iliyoko karibu na mlango wa hema la mkutano.

8. Kisha atayaondoa mafuta yote ya ng'ombe huyo: Mafuta yanayofunika matumbo,

9. figo mbili na mafuta yaliyo juu yake na yale yaliyo kiunoni, na yale yaliyoshikamana na figo na ini; hizi ni sehemu zilezile zinazoondolewa kwa mnyama wa sadaka ya amani.

10. Kuhani atazichukua na kuziteketeza juu ya madhabahu ya kuteketezea sadaka.

11. Lakini ngozi ya huyo ng'ombe, nyama, kichwa, miguu, matumbo na mavi yake,

12. yaani ng'ombe mzima aliyesalia atampeleka na kumteketeza nje ya kambi mahali safi ambapo majivu hutupwa, naye atamchoma kwa moto juu ya kuni; atachomwa moto hapo mahali pa kumwagia majivu.

13. “Iwapo jumuiya yote nzima ya Israeli imetenda dhambi bila ya kukusudia kwa kufanya kitu kilichokatazwa na amri ya Mwenyezi-Mungu

Walawi 4