Walawi 11:10-15 Biblia Habari Njema (BHN)

10. Lakini chochote kinachoishi baharini au mitoni, ambacho hakina mapezi wala magamba, yaani viumbe vyote viendavyo majini na viumbe vingine vyote viishivyo majini ni najisi kwenu.

11. Viumbe hivyo vitakuwa daima najisi kwenu. Msile nyama yao, wala msiiguse mizoga yao kwani ni najisi.

12. Chochote kinachoishi majini ambacho hakina mapezi na magamba ni najisi kwenu.

13. “Ndege wote wafuatao ni najisi kwenu; hivyo msile: Tai, furukombe, kipungu,

14. mwewe, aina zote za kozi,

15. aina zote za kunguru,

Walawi 11