Waebrania 7:20-26 Biblia Habari Njema (BHN)

20. Zaidi ya hayo, hapa pana kiapo cha Mungu. Wakati wale wengine walipofanywa makuhani hapakuwako kiapo.

21. Lakini Yesu alifanywa kuhani kwa kiapo wakati Mungu alipomwambia:“Bwana ameapa,wala hatabadili nia yake:‘Wewe ni kuhani milele.’”

22. Basi, kutokana na tofauti hii, Yesu amekuwa mdhamini wa agano lililo bora zaidi.

23. Tena: Hao makuhani wengine walikuwa wengi kwa sababu walikufa na hawakuweza kuendelea na kazi yao.

24. Lakini Yesu si kama wao, yeye anaishi milele; ukuhani wake hauondoki kwake.

25. Hivyo, yeye anaweza daima kuwaokoa kabisa wote wanaomwendea Mungu kwa njia yake, maana yeye anaishi milele kuwaombea kwa Mungu.

26. Basi, ilikuwa jambo la kufaa sana kwetu kuwa na kuhani kama huyo, mtakatifu, asiye na hatia wala dhambi ndani yake; ametenganishwa mbali na wenye dhambi, na ameinuliwa juu ya mbingu.

Waebrania 7