Waamuzi 20:23-25 Biblia Habari Njema (BHN)

23. Basi Waisraeli wakaenda juu, wakamlilia Mwenyezi-Mungu mpaka jioni. Kisha wakaomba shauri kwa Mwenyezi-Mungu: “Je, twende tena kupigana na ndugu zetu, wa kabila la Benyamini?” Mwenyezi-Mungu akawajibu, “Nendeni mkapigane nao.”

24. Hivyo siku ya pili Waisraeli wakakaribia kupigana na watu wa kabila la Benyamini.

25. Siku hiyo ya pili watu wa kabila la Benyamini walitoka Gibea na kuwashambulia Waisraeli, wakawaangusha chini Waisraeli 18,000.

Waamuzi 20