1. Baada ya hayo, nilimwona malaika mwingine akishuka kutoka mbinguni. Alikuwa na uwezo mkuu, na dunia ikamulikwa na mng'ao wake.
2. Basi, akapaza sauti kwa nguvu akisema, “Umeanguka; Babuloni mkuu umeanguka! Sasa umekuwa makao ya mashetani na pepo wachafu; umekuwa makao ya ndege wachafu na wa kuchukiza mno.
3. Maana mataifa yote yalileweshwa kwa divai kali ya uzinzi wake, nao wafalme wa dunia wamefanya uzinzi naye. Nao wafanyabiashara wa dunia wametajirika kutokana na anasa zake zisizo na kipimo.”
4. Kisha nikasikia sauti nyingine kutoka mbinguni ikisema,“Watu wangu, ondokeni kwake,ili msishirikiane naye katika dhambi zake,msije mkaipata adhabu yake.
5. Kwa maana dhambi zake zimekuwa nyingi mno,zimerundikana mpaka mbinguni,na Mungu ameyakumbuka maovu yake.
6. Mtendeeni kama alivyowatendea nyinyi;mlipeni mara mbili kwa yale aliyoyatenda.Mchanganyieni kikombeni mwake kinywaji kikali maradufu.
7. Mpeni mateso na uchungu kadiri ya kujigamba kwake,kulingana na kuishi kwake kwa anasa.Maana anajisemea moyoni: ‘Ninaketi hapa; mimi ni malkia.Mimi si mjane, wala sitapatwa na uchungu!’
8. Kwa sababu hiyo mabaa yake yatampata kwa siku moja:Ugonjwa, huzuni na njaa.Atachomwa moto,maana Bwana Mungu mwenye kumhukumu ana nguvu.”
9. Wafalme wa dunia waliofanya uzinzi naye na kuishi naye maisha ya anasa wataomboleza na kulia wakati watakapoona moshi wa mji huo unaoteketea.
10. Wanasimama kwa mbali kwa sababu ya kuogopa mateso yake na kusema, “Ole! Ole kwako Babuloni, mji maarufu na wenye nguvu! Kwa muda wa saa moja tu adhabu yako imekupata.”
11. Wafanyabiashara wa dunia watalia na kumfanyia matanga, maana hakuna mtu anayenunua tena bidhaa zao;