Nehemia 9:36-38 Biblia Habari Njema (BHN)

36. Na leo tumekuwa watumwa;tu watumwa katika nchi uliyowapa babu zetuwafurahie matunda na vipawa vyake vyema.

37. Kwa sababu ya dhambi zetu,utajiri wa nchi hiiunawaendea wafalme uliowaleta kututawala.Wanatutawala wapendavyohata na mifugo yetuwanaitendea wapendavyo,tumo katika dhiki kuu.”

38. Kutokana na haya yote yaliyotokea, sisi tunaweka agano imara na wakuu wetu kwa maandishi; Walawi na makuhani wanatia sahihi zao na mhuri wao.

Nehemia 9