Mwanzo 6:1-3 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Binadamu walipozidi kuongezeka duniani na kuzaa wasichana,

2. watoto wa kiume wa Mungu waliwaona hao wasichana wa watu kuwa ni wazuri, wakawachukua wale waliowapenda kuwa wake zao.

3. Hapo Mwenyezi-Mungu akasema, “Roho yangu haitakaa ndani ya binadamu milele, maana yeye ni wa kufa tu. Basi, hataishi zaidi ya miaka 120.”

Mwanzo 6