Mwanzo 47:1-2 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Basi, Yosefu akaenda kwa Farao, akamwambia, “Baba yangu na ndugu zangu pamoja na kondoo, ng'ombe na mali yao yote, wamefika kutoka nchi ya Kanaani. Sasa wako katika eneo la Gosheni.”

2. Yosefu alikuwa amewachukua ndugu zake watano, akawajulisha kwa Farao.

Mwanzo 47