Mwanzo 46:19-22 Biblia Habari Njema (BHN)

19. Raheli alimzalia Yakobo wana wawili: Yosefu na Benyamini.

20. Huko Misri, Asenathi, binti Potifera, aliyekuwa kuhani wa mji wa Oni, alimzalia Yosefu wana wawili: Manase na Efraimu.

21. Wana wa Benyamini walikuwa Bela, Bekeri, Ashbeli, Gera, Naamani, Ehi, Roshi, Mupimu, Hupimu na Ardi.

22. Watu hao kumi na wanne ni watoto na wajukuu wa Yakobo na Raheli, mkewe.

Mwanzo 46