28. Mungu akumiminie umande wa mbinguni;akupe ardhi yenye rutuba,nafaka na divai kwa wingi.
29. Jamii za watu zikutumikie,na mataifa yakuinamie kwa heshima.Uwe mtawala wa ndugu zako,watoto wa kiume wa mama yako wakuinamie kwa heshima.Kila akulaaniye na alaaniwe,kila akubarikiye na abarikiwe!”
30. Isaka alipokwisha kumbariki Yakobo, naye Yakobo alipokuwa ndio tu ametoka mbele ya baba yake Isaka, Esau kaka yake Yakobo, akarudi kutoka mawindoni.
31. Esau pia akatengeneza chakula kitamu, akampelekea baba yake, akamwambia, “Haya baba, inuka ule mawindo yangu mimi mwanao, ili upate kunibariki!”
32. Isaka akauliza, “Wewe ni nani?” Naye akamjibu, “Ni mimi mwanao Esau, mzaliwa wako wa kwanza.”