Mwanzo 10:25-32 Biblia Habari Njema (BHN)

25. Eberi alikuwa na watoto wa kiume wawili; wa kwanza akamwita Pelegi kwa sababu wakati huo watu duniani waligawanyika, na wa pili akamwita Yoktani.

26. Yoktani alikuwa baba wa Almodadi, Shelefu, Hasarmawethi, Yera,

27. Hadoramu, Uzali, Dikla,

28. Obali, Abimaeli, Sheba,

29. Ofiri, Hawila na Yobabu. Hao wote walikuwa watoto wa Yoktani.

30. Nchi walimokaa ilienea toka Mesha mpaka Sefari katika nyanda za juu za mashariki.

31. Hao ndio wazawa wa Shemu, kadiri ya makabila yao, lugha zao, nchi zao na mataifa yao.

32. Hao ndio jamaa za watoto wa Noa, kadiri ya vizazi vyao na mataifa yao. Kutokana nao mataifa yote yalienea duniani baada ya gharika.

Mwanzo 10