6. “Usituhubirie sisi.Mambo kama hayo si ya kuhubiriwa.Sisi hatutakumbwa na maafa!
7. Je, yafaa kusema hivyo, wazawa wa Yakobo?Je, Mwenyezi-Mungu ameacha uvumilivu wake?Je, yeye hufanya mambo kama haya?”Sivyo! Maneno yangu huwafaa watendao mambo mema.
8. Lakini Mwenyezi-Mungu awaambia hivi:“Nyinyi mnawavamia watu wangu kama adui.Mnawanyang'anya mavazi yao watu watulivu;watu wanaopita kwenda zao bila wasiwasi,na wasio na fikira zozote za vita.