Mika 1:1-3 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Neno la Mwenyezi-Mungu lilimjia Mika, mwenyeji wa Moreshethi, wakati Yothamu, Ahazi na Hezekia walipokuwa wafalme wa Yuda. Mika aliona mambo yote haya kuhusu Samaria na Yerusalemu.

2. Sikilizeni enyi watu wote;sikiliza ewe dunia na vyote vilivyomo.Mwenyezi-Mungu anakuja kuwashtaki,Bwana anena kutoka hekalu lake takatifu.

3. Naam! Mwenyezi-Mungu yuaja kutoka makao yake;atashuka na kutembea juu ya vilele vya dunia.

Mika 1