1. Neno la Mwenyezi-Mungu lilimjia Mika, mwenyeji wa Moreshethi, wakati Yothamu, Ahazi na Hezekia walipokuwa wafalme wa Yuda. Mika aliona mambo yote haya kuhusu Samaria na Yerusalemu.
2. Sikilizeni enyi watu wote;sikiliza ewe dunia na vyote vilivyomo.Mwenyezi-Mungu anakuja kuwashtaki,Bwana anena kutoka hekalu lake takatifu.
3. Naam! Mwenyezi-Mungu yuaja kutoka makao yake;atashuka na kutembea juu ya vilele vya dunia.