4. “Yeyote aliye mjinga na aje hapa!”Na yeyote aliye mpumbavu humwambia:
5. “Njoo ukale chakula,na unywe divai niliyotengeneza.
6. Achana na ujinga upate kuishi;fuata njia ya akili.”
7. Anayemkosoa mwenye dharau hupata matusi,amkaripiaye mwovu huishia kwa kuumizwa.
8. Usimwonye mwenye dharau maana atakuchukia;mwonye mwenye hekima naye atakupenda.
9. Mfunze mwenye hekima naye atazidi kuwa na hekima;mfundishe mwadilifu naye atazidi kuelimika.
10. Kumcha Mwenyezi-Mungu ni msingi wa hekima;na kumjua yule Mtakatifu ni kupata akili.