3. Amewatuma watumishi wake wa kike mjini,waite watu kutoka kwenye vilele vya miinuko:
4. “Yeyote aliye mjinga na aje hapa!”Na yeyote aliye mpumbavu humwambia:
5. “Njoo ukale chakula,na unywe divai niliyotengeneza.
6. Achana na ujinga upate kuishi;fuata njia ya akili.”
7. Anayemkosoa mwenye dharau hupata matusi,amkaripiaye mwovu huishia kwa kuumizwa.
8. Usimwonye mwenye dharau maana atakuchukia;mwonye mwenye hekima naye atakupenda.