Methali 9:1-9 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Hekima amejenga nyumba yake,nyumba yenye nguzo saba.

2. Amechinja wanyama wa karamu,divai yake ameitayarisha,ametandika meza yake.

3. Amewatuma watumishi wake wa kike mjini,waite watu kutoka kwenye vilele vya miinuko:

4. “Yeyote aliye mjinga na aje hapa!”Na yeyote aliye mpumbavu humwambia:

5. “Njoo ukale chakula,na unywe divai niliyotengeneza.

6. Achana na ujinga upate kuishi;fuata njia ya akili.”

7. Anayemkosoa mwenye dharau hupata matusi,amkaripiaye mwovu huishia kwa kuumizwa.

8. Usimwonye mwenye dharau maana atakuchukia;mwonye mwenye hekima naye atakupenda.

9. Mfunze mwenye hekima naye atazidi kuwa na hekima;mfundishe mwadilifu naye atazidi kuelimika.

Methali 9