6. Makaripio ya rafiki yaonesha uaminifu,lakini busu la adui ni udanganyifu.
7. Aliyeshiba hata asali huikataa,lakini kwa mwenye njaa kila kichungu ni kitamu.
8. Mtu aliyepotea mbali na kwake,ni kama ndege aliyepotea mbali na kiota chake.
9. Mafuta na manukato huufurahisha moyo,lakini taabu hurarua roho.
10. Usisahau rafiki zako wala wa baba yako.Ukipatwa na janga usikimbilie kwa nduguyo;afadhali jirani aliye karibu kuliko ndugu aliye mbali.
11. Uwe na hekima mwanangu upate kunifurahisha moyo,nami sitakosa la kumjibu yeyote anayenilaumu.
12. Mwenye busara huona hatari akajificha,lakini mjinga hujitokeza mbele akaumia.
13. Mtu akiahidi mbele yako kumdhamini mgeni, chukua nguo yake;mfanye awajibike kwa kuwadhamini wageni.
14. Amwamkiaye jirani kwa kelele alfajiri,itaeleweka kwamba amemtakia laana.
15. Mke mgomvi daima,ni sawa na tonatona ya maji siku ya mvua.
16. Kumzuia ni sawa na kuzuia upepo,au kukamata mafuta kwa mkono.