1. Afadhali mkate mkavu kwa amani,kuliko karamu katika nyumba ya ugomvi.
2. Mtumwa mwenye busara atachukua nafasi ya mwana mpumbavu,atapata sehemu ya urithi wa jamaa hiyo.
3. Ubora wa dhahabu ama fedha hupimwa kwa moto,lakini Mwenyezi-Mungu ndiye apimaye mioyo ya watu.
4. Mtenda maovu husikiliza maneno mabaya,mwongo hutegea sikio ulimi mdanganyifu.
5. Anayemdhihaki maskini anamtukana Muumba wake;anayefurahia maafa hatakosa kuadhibiwa.