29. Nawaambieni, sitakunywa tena divai ya zabibu mpaka siku ile nitakapoinywa mpya pamoja nanyi katika ufalme wa Baba yangu.”
30. Baada ya kuimba wimbo, wakaondoka, wakaenda katika mlima wa Mizeituni.
31. Kisha Yesu akawaambia, “Usiku huu wa leo, nyinyi nyote mtakuwa na mashaka nami, maana Maandiko Matakatifu yasema:‘Nitampiga mchungaji,na kondoo wa kundi watatawanyika.’
32. Lakini baada ya kufufuka kwangu, nitawatangulieni Galilaya.”