Mathayo 13:42-45 Biblia Habari Njema (BHN)

42. na kuwatupa katika tanuri ya moto, na huko watalia na kusaga meno.

43. Kisha, wale wema watangara kama jua katika ufalme wa Baba yao. Mwenye masikio na asikie!

44. “Ufalme wa mbinguni unafanana na hazina iliyofichika shambani. Mtu mmoja aliigundua, akaificha tena. Alifurahi sana hata akaenda kuuza yote aliyokuwa nayo, akalinunua shamba lile.

45. “Tena, ufalme wa mbinguni unafanana na mfanyabiashara mmoja mwenye kutafuta lulu nzuri.

Mathayo 13