Mathayo 11:1-4 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Yesu alipomaliza kuwapa wanafunzi kumi na wawili maagizo, alitoka hapo, akaenda kufundisha na kuhubiri katika miji yao.

2. Yohane Mbatizaji akiwa gerezani alipata habari juu ya matendo ya Kristo. Basi, Yohane akawatuma wanafunzi wake,

3. wamwulize: “Je, wewe ni yule anayekuja, au tumngoje mwingine?”

4. Yesu akawajibu, “Nendeni mkamwambie Yohane mambo mnayoyasikia na kuyaona:

Mathayo 11