29. Yampasa kuinama na kujinyenyekesha,huenda ikawa tumaini bado lipo.
30. Yampasa kumgeuzia shavu mwenye kumpiga,na kuwa tayari kupokea matusi yake.
31. Mwenyezi-Mungu hatatutupa milele.
32. Ingawa atufanya tuhuzunike,atakuwa na huruma tenakadiri ya wingi wa fadhili zake.
33. Yeye hapendelei kuwatesawala kuwahuzunisha wanadamu.
34. Wafungwa wote nchiniwanapodhulumiwa na kupondwa;
35. haki za binadamu zinapopotoshwambele yake Mungu Mkuu,
36. kesi ya mtu inapopotoshwa mahakamani,je, Mwenyezi-Mungu haoni hayo?
37. Nani awezaye kuamuru kitu kifanyikeMwenyezi-Mungu asipopanga iwe hivyo?
38. Maafa na mema hutokea tukwa amri yake Mungu Mkuu.
39. Kwa nini mtu anung'unike,ikiwa ameadhibiwa kwa dhambi zake?