Maombolezo 3:29-39 Biblia Habari Njema (BHN)

29. Yampasa kuinama na kujinyenyekesha,huenda ikawa tumaini bado lipo.

30. Yampasa kumgeuzia shavu mwenye kumpiga,na kuwa tayari kupokea matusi yake.

31. Mwenyezi-Mungu hatatutupa milele.

32. Ingawa atufanya tuhuzunike,atakuwa na huruma tenakadiri ya wingi wa fadhili zake.

33. Yeye hapendelei kuwatesawala kuwahuzunisha wanadamu.

34. Wafungwa wote nchiniwanapodhulumiwa na kupondwa;

35. haki za binadamu zinapopotoshwambele yake Mungu Mkuu,

36. kesi ya mtu inapopotoshwa mahakamani,je, Mwenyezi-Mungu haoni hayo?

37. Nani awezaye kuamuru kitu kifanyikeMwenyezi-Mungu asipopanga iwe hivyo?

38. Maafa na mema hutokea tukwa amri yake Mungu Mkuu.

39. Kwa nini mtu anung'unike,ikiwa ameadhibiwa kwa dhambi zake?

Maombolezo 3