Maombolezo 3:17-26 Biblia Habari Njema (BHN)

17. Moyo wangu haujui tena amani,kwangu furaha ni kitu kigeni.

18. Nimewaza “Nimekata tamaa kabisa,tumaini langu kwa Mwenyezi-Mungu limetoweka.”

19. Kukumbuka taabu na kutangatanga kwangukwanipa uchungu kama wa nyongo.

20. Nayafikiria hayo daima,nayo roho yangu imejaa majonzi.

21. Lakini nakumbuka jambo hili moja,nami ninalo tumaini:

22. Kwamba fadhili za Mwenyezi-Mungu hazikomi,huruma zake hazina mwisho.

23. Kila kunapokucha ni mpya kabisa,uaminifu wake ni mkuu mno.

24. Mwenyezi-Mungu ndiye hazina yanguhivyo nitamwekea tumaini langu.

25. Mwenyezi-Mungu ni mwema kwa wanaomtegemea,ni mwema kwa wote wanaomtafuta.

26. Ni vema mtu kungojea kwa saburiukombozi utokao kwa Mwenyezi-Mungu.

Maombolezo 3