13. Alinichoma moyoni kwa mishale,kutoka katika podo lake.
14. Nimekuwa kitu cha dhihaka kwa watu wote,mchana kutwa nimekuwa mtu wa kuzomewa.
15. Amenijaza taabu,akanishibisha uchungu.
16. Amenisagisha meno katika mawe,akanifanya nigaegae majivuni.
17. Moyo wangu haujui tena amani,kwangu furaha ni kitu kigeni.
18. Nimewaza “Nimekata tamaa kabisa,tumaini langu kwa Mwenyezi-Mungu limetoweka.”