Maombolezo 2:1-3 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Mwenyezi-Mungu, kwa hasira yake,amewaweka watu wa Siyoni gizani.Fahari ya Israeli ameibwaga chini.Siku ya hasira yakealilitupilia mbali hata hekalu lake.

2. Mwenyezi-Mungu ameharibu bila hurumamakazi yote ya wazawa wa Yakobo.Kwa ghadhabu yake amezibomoa ngome za watu wa Yuda.Ufalme wao na watawala wakeameuporomosha chini kwa aibu.

3. Nguvu yote ya Israeli ameivunja kwa hasira.Hakunyosha mkono kuwasaidiawalipokutana na adui;amewawakia watu wa Yakobo kama moto,akateketeza kila kitu.

Maombolezo 2