1. Ajabu mji uliokuwa umejaa watu,sasa wenyewe umebaki tupu!Ulikuwa maarufu kati ya mataifa;sasa umekuwa kama mama mjane.Miongoni mwa miji ulikuwa kama binti mfalme;sasa umekuwa mtumwa wa wengine.
2. Walia usiku kucha;machozi yautiririka.Hakuna hata mmoja wa wapenzi wake wa kuufariji.Rafiki zake wote wameuhadaa;wote wamekuwa adui zake.
3. Watu wa Yuda wamekwenda uhamishonipamoja na mateso na utumwa mkali.Sasa wanakaa miongoni mwa watu wa mataifa,wala hawapati mahali pa kupumzika.Waliowafuatia wamewakamata wakiwa taabuni.