15. “Lakini kama hamtaitii sauti ya Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu, au msipokuwa waangalifu kutekeleza amri zake zote na masharti ninayowaamuru leo, basi mtapatwa na laana hizi zote:
16. Mtapata laana katika miji yenu na mashamba yenu.
17. Vikapu vyenu vya nafaka vitalaaniwa na vyombo vyenu vya kukandia mkate.
18. Watoto wenu watalaaniwa na mazao yenu ya nchi; mifugo yenu italaaniwa isiongezeke.