Kumbukumbu La Sheria 28:15-18 Biblia Habari Njema (BHN)

15. “Lakini kama hamtaitii sauti ya Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu, au msipokuwa waangalifu kutekeleza amri zake zote na masharti ninayowaamuru leo, basi mtapatwa na laana hizi zote:

16. Mtapata laana katika miji yenu na mashamba yenu.

17. Vikapu vyenu vya nafaka vitalaaniwa na vyombo vyenu vya kukandia mkate.

18. Watoto wenu watalaaniwa na mazao yenu ya nchi; mifugo yenu italaaniwa isiongezeke.

Kumbukumbu La Sheria 28