Kumbukumbu La Sheria 25:14-18 Biblia Habari Njema (BHN)

14. Wala msiwe na aina mbili za vipimo vya kupimia, kubwa na ndogo.

15. “Tumieni mizani na vipimo vyenye uzito sahihi ili mpate kuishi maisha marefu katika nchi anayowapa Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu.

16. Wote wanaofanya mambo hayo, wote wanaotenda kwa udanganyifu ni chukizo kwa Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu.

17. “Kumbukeni kitendo cha Waamaleki mlipokuwa safarini kutoka Misri.

18. Kumbukeni walivyowashambulieni huko njiani mkiwa wanyonge na kuwapiga wale wote waliokuja nyuma yenu wamechoka. Waamaleki hawakumwogopa Mungu.

Kumbukumbu La Sheria 25