Kumbukumbu La Sheria 22:12-17 Biblia Habari Njema (BHN)

12. “Funga vishada katika pembe nne za vazi lako.

13. “Mwanamume akioa mwanamke, halafu baadaye akate shauri kumwacha,

14. na kumshtaki kwamba ametenda mambo ya aibu, na kumharibia sifa kwa kusema kwamba hakupata ushahidi wa ubikira wakati alipomwoa,

15. basi, wazazi wa mwanamke huyo watachukua ushahidi wa ubikira wa binti yao kwa wazee kwenye lango la mji na kuwaambia,

16. ‘Tulimwoza binti yetu kwa mtu huyu, lakini sasa hamtaki tena,

17. na ajabu ni kwamba amemshtaki mambo ya aibu na kusema ati hakumkuta na ushahidi wowote wa ubikira. Hata hivyo ushahidi wa ubikira wa binti yetu ni huu.’ Halafu atakunjua nguo yenye huo ushahidi mbele ya wazee wa mji.

Kumbukumbu La Sheria 22