Kumbukumbu La Sheria 2:16-20 Biblia Habari Njema (BHN)

16. “Basi, watu hao wote wenye umri wa kwenda vitani walipokwisha aga dunia,

17. Mwenyezi-Mungu aliniambia,

18. ‘Leo hii mtauvuka mpaka wa Moabu kwa kupitia nchi ya Ari.

19. Mtaifikia nchi ya Waamoni. Msiwasumbue wala msipigane nao kwa kuwa sitawapeni sehemu yoyote ya hao wazawa wa Amoni; iwe mali yenu. La! Hao ni wazawa wa Loti, na nimewapa hiyo nchi iwe mali yao.’”

20. (Nchi hiyo inajulikana pia kama nchi ya Warefai. Warefai walikuwa wanaishi huko hapo zamani; Waamoni waliwaita hao Wazamzumi.

Kumbukumbu La Sheria 2