1. Mwenyezi-Mungu asema;“Nilikuwa tayari kujioneshakwao wasiouliza habari zangu.Nilikuwa tayari kuwapokeawale wasionitafuta.Nililiambia taifa ambalo halikuomba kwa jina langu:‘Nipo hapa! Nipo hapa!’
2. Mchana kutwa niliwanyoshea mikono watu waasi,watu ambao hufuata njia zisizo sawa,watu ambao hufuata fikira zao wenyewe.
3. Ni watu ambao daima hunichokoza waziwazi;hutambikia miungu yao katika bustani,na kuifukizia ubani juu ya matofali.
4. Huketi makaburini na kukaa mafichoni usiku.Hula nyama ya nguruwe na mchuzi wa wanyama haramu.
5. Huwaambia wale wanaokutana nao:‘Kaeni mbali nami;msinikaribie kwani mimi ni mtakatifu!’Watu hao wananikasirisha mno,hasira yangu ni kama moto usiozimika.