Isaya 49:1-4 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Nisikilizeni, enyi nchi za mbali,tegeni sikio, enyi watu wa mbali!Mwenyezi-Mungu aliniita kabla sijazaliwa,alitaja jina langu nikiwa tumboni mwa mama yangu.

2. Aliyapa ukali maneno yangu kama upanga mkali,alinificha katika kivuli cha mkono wake;aliufanya ujumbe wangu mkali kama ncha ya mshale,akanificha katika podo lake.

3. Aliniambia, “Wewe ni mtumishi wangu;kwako, Israeli, watu watanitukuza.”

4. Lakini mimi nikafikiri,“Nimeshughulika bure,nimetumia nguvu zangu bure kabisa.”Hata hivyo, Mwenyezi-Mungu atanipa haki yangu;tuzo la kazi yangu liko kwa Mungu.

Isaya 49