17. Wote wanaotegemea sanamu za miungu,wote wanaoziambia: Nyinyi ni miungu yetu;watakomeshwa na kuaibishwa.
18. “Sikilizeni enyi viziwi!Tazameni enyi vipofu, mpate kuona!
19. Nani aliye kipofu ila mtumishi wangu?Nani aliye kiziwi kama mjumbe ninayemtuma?Ni nani aliye kipofu kama huyu niliyemweka wakfu,au kipofu kama mtumishi wa Mwenyezi-Mungu?