Isaya 40:26-31 Biblia Habari Njema (BHN)

26. Inueni macho yenu juu mbinguni!Je, ni nani aliyeziumba nyota hizo?Ni yule aziongozaye kama jeshi lake,anayeijua idadi yake yote,aziitaye kila moja kwa jina lake.Kwa sababu yeye ni mwenye nguvu nyingi,hakuna hata moja inayokosekana.

27. Enyi watu wa Israeli wazawa wa Yakobo,kwa nini mnalalamika na kusema:“Mwenyezi-Mungu hatujali sisi!Mungu wetu hajali haki yetu!”

28. Je, nyinyi bado hamjui?Je, hamjapata kusikia?Mwenyezi-Mungu ndiye Mungu wa milele;yeye ndiye Muumba wa kila kitu duniani.Yeye hafifii kamwe wala kuishiwa nguvu.Maarifa yake hayachunguziki.

29. Yeye huwapa uwezo walio hafifu,wanyonge huwapa nguvu.

30. Hata vijana watafifia na kulegea;naam, wataanguka kwa uchovu.

31. Lakini wote wanaomtumainia Mwenyezi-Mungu,watapata nguvu mpya.Watapanda juu kwa mabawa kama tai;watakimbia bila kuchoka;watatembea bila kulegea.

Isaya 40