Isaya 31:5-9 Biblia Habari Njema (BHN)

5. Kama ndege arukavyo juu ya viota vyake,ndivyo Mwenyezi-Mungu atakavyoulinda Yerusalemu,ataulinda na kuukomboa,atauhifadhi na kuuokoa.

6. Enyi Waisraeli,mrudieni huyo mliyemsaliti vibaya.

7. Wakati utafika ambapo nyotemtavitupilia mbali vinyago vyenuvya fedha na dhahabu ambavyommejitengenezea kwa mikono yenu,vikawakosesha.

8. Hapo Waashuru watauawa kwa upanga,lakini si kwa upanga wa binadamu;naam, wataangamizwa kwa upangaambao ni zaidi ya ule wa binadamu.Waashuru watakimbiana vijana wao watafanyizwa kazi za kitumwa.

9. Mfalme wao atatoroka kwa hofu,na maofisa wao wataiacha bendera yao kwa woga.Hayo ameyatamka Mwenyezi-Munguambaye moto wake umo mjini Siyoni,naam, tanuri lake limo mjini Yerusalemu.”

Isaya 31