Isaya 3:17-24 Biblia Habari Njema (BHN)

17. Basi, mimi Mwenyezi-Mungu nitawaadhibu;nitawanyoa nywele hao wanawake wa Siyoni,na kuwavua nguo za kufunika uchi wao.”

18. Siku yaja ambapo Mwenyezi-Mungu atawanyanganya wanawake wa Yerusalemu vitu vyote wanavyoringia: Njuga, kaya, mikufu,

19. vipuli, vikuku, shungi,

20. vitambaa vya kichwani, bangili, vibwebwe, vibweta vya marashi, hirizi,

21. pete, hazama,

22. mavazi ya sikukuu, mitandio, majoho, mikoba,

23. mavazi yaoneshayo, mavazi ya kitani, vilemba na shela.

24. Badala ya kunukia marashi watatoa uvundo;badala ya mishipi mizuri watatumia kamba;badala ya nywele nzuri watakuwa na upara;badala ya mavazi mazuri watavaa matambara;uzuri wao wote utageuka kuwa aibu.

Isaya 3